-->

Mtandao wa Wikileaks wafichua hotuba ya Clinton

Mtandao wa Wikileaks, umechapisha kile unachosema kuwa hotuba ya kibinafsi ya Bi Hillary Clinton, kwa wakuu na wanaharakati. Katika mojawapo ya hotuba, ameziambia benki nchini Marekani kuwa ziko katika nafasi nzuri mno ya kuleta mabadiliko katika sekta ya kifedha, huku katika hotuba nyengine akisema kuwa anaunga mkono biashara huru ya wazi ndani na nje ya nchi. Bi Clinton amekataa kuchapisha hotuba hizo, iliyompa mamilioni ya dola kabla ya kuwa mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya chama cha Democratic. Mpinzani wake katika chama cha Democrat wakati huo Bernie Sanders alikuwa amemtaka kutoa nakala za hotuba hiyo ,ambazo zinadaiwa kumpatia dola milioni 26. Ufichuzi huo wa Wikileaks huenda ukatawala habari wikendi hii huku wachanganuzi na wanasiasa wakibashiri kwamba hatua hiyo itawapendelea waliokuwa wagombea Marco Rubio,Jeb Bush na hata Ted Cruz.

Nemo enim ipsam voluptatem quia voluptas sit aspernatur aut odit aut fugit, sed quia consequuntur magni dolores eos qui ratione voluptatem sequi nesciunt.

Disqus Comments