-->

Facebook yazindua mtandao wa kutumika kazini

Facebook imenzisha mfumo mpya wa mtandao unaojulikana kama Workplace, ambao utaziwezesha kampuni kubuni njia ya kufanya mawasiliano. Mtandao huo unaofanana na wa Facebook, na ulio na sehemu muhimu zikiwemo za kupeperusha video moja kwa moja na kwa mawasiliano ya ujumbe, hauwezi kutumiwa na mtu binafsi. Mtandao huo umebuniwa kuchuchukua mahala pa mifumo mingine kama ya email kwa mawasiliano kazini. Mdadisi mmoja alisema kuwa mtandao huo utatoa ushindani mkubwa kwa mifumo mingine washindani. Utaingia kwenye masoko sawa na ya mtandao wa Microsoft wa Yammer, ambao makampuni yanaweza kutumia na ule wa Slack ambao ni wa mawasiliano ya ujumbe. Facebook imekuwa ikiufanyia majaribio mfumo huo ambao awali ulifahamika kama Facebook at Work, kwa muda wa miaka miwili na kusema kuwa hadi makampuni 1000 tayari yanautumia.

Nemo enim ipsam voluptatem quia voluptas sit aspernatur aut odit aut fugit, sed quia consequuntur magni dolores eos qui ratione voluptatem sequi nesciunt.

Disqus Comments