-->

DR Congo imo kwenye 'hatari kubwa', UN yaonywa

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inakabiliwa na hatari kubwa ya kutumbukia kwenye machafuko, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetahadharishwa. Mjumbe wa UN Maman Sidikou amesema wanajeshi 18,000 wa kulinda amani wa umoja huo ambao wamo nchini humo hawana uwezo wa kukabiliana na ghasia kama hizo iwapo zitazuka. Maandamano yenye umwagikaji wa damu yamekuwa wakishuhudiwa mara kwa mara kufuatia hatua ya kuahirishwa kwa tarehe ya uchaguzi wa rais. Upinzani unamtuhumu Rais Joseph Kabila kwa kujaribu kukwamilia mamlaka hata baada ya kumalizika kwa muhula wake Desemba. Watu kadha walifariki wakati wa maandamano ya kupinga serikali mwezi jana mjini Kinshasa baada ya tume ya uchaguzi kusema haingewezekana uchaguzi ufanyike Novemba. 'Watu 50 wauawa' maandamano ya upinzani DR Congo Marekani yazuilia mali ya maafisa wawili wa DR Congo Makao makuu ya vyama vitatu vya upinzani yalishambuliwa na kuchomwa moto. "Wadau kutoka pande zote wanaonekana kuwa tayari zaidi na kutumia ghasia kutimiza malengo yao," Bw Sidikou, mkuu wa kikosi cha kulinda amani cha UN kunachojulikana kama Monusco, aliambia baraza la usalama la UN Jumanne. Image copyright Reuters Image caption Rais Joseph Kabila haruhusiwi kuwania urais tena "Ingawa Monusco itafanya kila iwezalo kulinda raia, haina uwezo wa kukabiliana na hatari zote zilizopo." Aliongeza: "Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeingia kipindi cha hatari kubwa kwa uthabiti wake. Kipindi kijacho kitakuwa kigumu sana, kuna uwezekano wa kufikia pahala ambapo ghasia zitazidi." DR Congo haijawahi kuwa na rais aliyekabidhi madaraka kwa njia ya amani kwa mrithi wake tangu uhuru miaka 55 iliyopita. Bw Kabila aliingia madarakani 2001 baada ya kuuawa kwa babake Laurent Kabila.

Nemo enim ipsam voluptatem quia voluptas sit aspernatur aut odit aut fugit, sed quia consequuntur magni dolores eos qui ratione voluptatem sequi nesciunt.

Disqus Comments